Genesis 39:2-6

2Bwana alikuwa pamoja na Yusufu, naye akastawi, Yusufu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri. 3Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yusufu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya, 4Yusufu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho. 5Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yusufu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yusufu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani. 6Kwa hiyo Potifa akamwachia Yusufu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yusufu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula.

Yusufu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
Copyright information for SwhKC